Chama cha Wananchi au Civic United Front (CUF) ni chama cha kisiasa nchini Tanzania. CUF ni chama cha uliberali wa kidemokrasia ambacho kauli mbiu yake ni Haki Sawa kwa Wote na Sera yake Kuu ni Utajirisho. CUF inasimamia elimu bora, afya madhubuti, mfumo adilifu wa kodi, Muungano wa haki, siasa kuwa utumishi ulioutukuka kwa umma na fursa sawa katika kujiendeleza kiuchumi, kijamii na kisiasa.














